Ads 468x60px

Saturday, January 18, 2014

DIAMOND PLATNUMZ - HE'S LIVING BIG (NDINGA MPYA + SWIMMING POOL CONSTRUCTION @ HIS NEW HOME)

DIAMOND & HIS NEW RIDE
Diamond Plutnumz he's living like how stars wanatakiwa kuishi, kwanza anajipenda, ana jijali na ana ogopa kushuka kimziki na kimafanikio.
Na ndio maana huyu jamaa anafanikiwa sana kwa upande wote wa muziki na maisha ya kawaida, anapenda kujiwekea ili kesho asi aibike, kila anapopata bahati ya kusafiri nje ya tanzania, anapenda kuitumia fursa vilivyo.
Hapo ni muonekano wa ujenzi wa swimming pool nyumbani kwake Platnumz ambako anapasubiri kwa hamu sana kwani bado ana endelea na ujenzi!
Go getta bro...Kila kheri....wakilisha TZAs abroad wafahamu kuwa na sisi WE CAN!

Wednesday, January 15, 2014

DJCHOKA: HIZI NDIZO SABABU ZANGU KWANINI NIMEPUMZIKA KAZI YA UDJ

Leo naomba niwatangazie wadau wangu na mashabiki wote waliokuwa wakinipenda kipindi nikiwa nawadj wasanii wa hapa nchini na hata wale wasanii waliokuwa wakitoka nje ya bongo. Natangaza rasmi kupumzika kazi hii ya uDJ niliyoanza nayo toka 2005 mpaka leo, sababu za kupumzika nimeona nipumzishe uDJ niendelee na kazi inayoniingizia kipato nazungumzia website yangu hii tokea ikiwa ni blog.

Kazi ya kudj wasanii ni kazi fulani nzuri lakini ni ngumu sana usipokuwa na hobby nayo, nimeifanya kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe yakupenda mziki na sikuwahi kulalamika mslahi ninayoyapata kwasababu niliifanya kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe hata napokuwa jukwaani nilikuwa nafurahia sana. Lakini kwa kuwa kazi hii ya kuandika habari na kuonyesha kazi za wasanii wa hapa nchini ndio inayonilipa vizuri basi naona sina budi kupumzisha kimoja ili niendelee na kimoja

Baada ya kupumzisha kazi yakudj kwenye majukwaa na kuwadj wasanii sasa nitakuwa naendelea na kazi yakuvumbua vipaji vya wasanii pia nitaendelee na mix tape zangu kama kawaida. Msanii atakayenihitaji sasa hivi basi ujue itakuwa kazi yakwenda kupiga picha show zake au kurecord show zake TU akiwa jukwaani. Mbali na hapo nitaendelea kupromoti mziki wa nyumbani na wasanii wake mpaka mwisho wangu. Nawakaribisha madj wadogo ambao mlipenda kuwa madj wa wasanii na hamkujua jinsi yakuanzia, nitawashauri na pia nitawafundisha njia za kuwadj wasanii hususani wasanii wa Hip Hop na Bongo Fleva unacheza nao vipi unapokuwa nao jukwaani.
Nawapenda sana wadau wote wa DJCHOKA MUSIC kwasababu bila nyie hakuna mimi
ONE
DJ CHOKA

MCHOMVU, B12 & DIVA ''OUT OF CLOUDS''




WATANGAZAJI maarufu Bongo wa Redio Clouds Fm ya jijini Dar es
Salaam, Hamisi Mandi ‘B 12’, Adam Mchomvu na Loveness Malinzi
‘Diva’, wamepigwa chini na kituo hicho, Risasi Mchanganyiko
linakupa zaidi.
Habari za chini kwa chini kutoka kwa chanzo chetu zinasema kuwa,
uongozi wa Clouds umefikia hatua hiyo baada ya kuchoshwa na
tabia ya utovu wa nidhamu kwa watangazaji hao.
Hata hivyo, madai ya mitaani yanasema kwamba, watangazaji hao
wamesimamishwa kwa kosa la kukacha sherehe za maadhimisho
ya Miaka 14 ya Clouds FM, yaliyofanyikia hivi karibuni katika
Viwanja vya Mwembeyanga, Temeke, Dar.

Risasi Mchanganyiko lilimvutia waya, Mkurugenzi wa Vipindi na
Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Muhatahaba na kumwuliza
juu ya ishu hiyo ambapo alikiri.
“Ni kweli tumefikia uamuzi wa kuwasimamisha B 12, Diva na
Mchomvu baada ya kukiuka baadhi ya makubaliano baina yao na
ofisi, hivyo kusababisha usumbufu mkubwa ambao ulitulazimu
kuingia gharama ambazo hazikutarajiwa.
“Hatutakuwa nao kwa muda usiojulikana, ingawa watu wengi
wamekuwa wakinihoji juu ya hilo lakini watachotakiwa kuelewa ni
kwamba hakuna ofisi isiyokuwa na sheria na taratibu za kuongoza
watu wake, sasa hao wamevunja taratibu zetu,” alisema Ruge bila
kufafanua zaidi.
Alipoulizwa ni taratibu zipi watangazaji hao walizovunja alisema:
“Nashindwa kueleza kosa la kila mmoja ila naomba nieleweke kuwa
hao watangazaji kwa sasa tumewasimamisha kwa muda usijulikana
wakati tukifikiria cha kufanya. Muhimu hapo ni kwamba
wamekwenda kinyume na tulivyokubaliana.”
 

Facebook and Twitter

Promo Sites